SHABANA NDIO WAKULAUMIWA
Gor Mahia FC wameilaumu Shabana FC kwa visa viovu vilivyoshuhudiwa katika uwanja wa Gusii siku ya Jumapili, wakielezea ghasia hizo kuwa “aibu kwa soka ya Kenya.”
Katika taarifa yenye maneno iliyotolewa Jumatatu, klabu hiyo ilishutumu Shabana, timu ya nyumbani, kwa kukosa kuhakikisha usalama ufaao kwa mechi ambayo ilikuwa imeripotiwa kuwa hatari.
Klabu hiyo pia ilifichua kuwa wafuasi wake kadhaa walipata majeraha mabaya, ikidai kuwa mashambulizi hayo yalionekana kuwa yamepangwa.
Gor Mahia pia walitilia shaka jinsi mechi hiyo ilivyoruhusiwa kuendelea, licha ya ushauri kutoka kwa vyombo vya usalama vya eneo hilo.
Kulingana na klabu hiyo, Afisa Mkuu wa Idara ya Polisi (OCPD) katika Kaunti Ndogo ya Kisii alikuwa ameshauri dhidi ya mechi hiyo kuendelea, akitaja mazingira tete.
Imetayarishwa na Nelson Andati
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































