#Basketball #Sports

OLUOCH AOMBOLEZA PAUL OTULA

Kocha mkuu wa mpira wa vikapu wa timu ya Chuo Kikuu cha Africa Nazarene Michael Oluoch amemuomboleza marehemu rais wa Shirikisho la Mpira wa Kikapu nchini Paul Otula, akimtaja kama nguzo katika chama cha mpira wa vikapu nchini.

Oluoch anasema kufariki kwa Otula sio tu pigo kwa udugu wa mpira wa vikapu bali kwa taasisi ya mafunzo ya mchezo huo.

Otula, ambaye aliaga dunia Alhamisi iliyopita baada ya kupatwa na mshtuko wa moyo nyumbani kwake Nairobi, pia aliwahi kuwa mwalimu Mkuu wa Shule ya upili ya Maseno.

Imetayarishwa na Nelson Andati

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *