#Local News #uncategorized

MADAI YA OMTATAH YAIBUA UTATA BUSIA

Afisi ya gavana wa Busia Paul Otuoma imekanusha madai ya kutumia visivyo shilingi bilioni 5 za bajeti ya mwaka wa kifedha wa 2022-23 jinsi ilivyoibuliwa na seneta wa kaunti hiyo Okiya Omtatah.

Kupitia taarifa kwa vyombo vya habari, afisi hiyo imemtaka Omtatah kuomba msamaha kutokana na kauli zake la sivyo achukuliwe hatua za kisheria.

Hata hivyo kulingana na seneta huyo, afisi ya gavana Otuoma ilipenyeza matumizi ya ziada kwenye bajeti hiyo licha ya kutokuwepo kwenye bajeti ya awali.

Imetayarishwa na Antony Nyongesa

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *