“MUUAJI” WA IKULU KUZUILIWA KWA SIKU 14
Mshukiwa wa mauaji ya afisa wa GSU nje ya Ikulu ya Nairobi Kithuka Musyimi, atazuiliwa kwa siku 14 zaidi ili kuruhusu polisi kukamilisha uchunguzi katika kifo cha afisa huyo aliyeuawa kwa kudungwa mshale.
Sehemu ya uchunguzi inahusisha ukaguzi wa mienendo ya mshukiwa na mawasiliano ya simu yake, duru zikiarifu kuwa Musyimi na afisa huyo kwa jina Ramadhan Hamisi waliwahi kukutana mara kadhaa kabla ya siku ya tukio.
Hamisi alizikwa nyumbani kwao kaunti ya Kajiado hapo jana.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































