SERIKALI HUZIMA UMEME, RUTO
Umeme ambao umekuwa ukipotea katika baadhi ya maeneo nchini kati ya saa kumi na moja jioni na saa nne usiku umekuwa ukizimwa na serikali kutokana na mahitaji ya juu ya umeme ambayo serikali haiwezi kutosheleza.
Haya ni kwa mujibu wa rais William Ruto kwenye kikao na wakenya wanaoishi nchini Qatar, akisema Kenya inahitaji zaidi ya shilingi trilioni 1 kuongeza umeme utakaotosha mahitaji hayo.
Aidha, amewahimiza wakenya kuchangia maendeleo ya taifa bila serikali kuchukua madeni ya kigeni.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































