SERIKALI YASISITIZA UMEME UPO
Serikali imewaondolea wakenya hofu ya uhaba wa nguvu za umeme ambao kwa mujibu wa Rais William Ruto, umesababisha kuzimwa kwa umeme katika baadhi ya maeneo majira ya jioni ili kukidhi mahitaji mengi ya bidhaa hiyo.
Kulingana na katibu mkuu katika wizara ya kawi Alex Wacira, taifa lina nguvu za umeme za kutosha, na kauli ya rais ililenga tu kuhimiza uzalishaji zaidi wa nguvu hizo.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































