GOR MAHIA YALENGA KUREJEA NJIA YA MATAJI
Klabu ya Gor Mahia, ambayo bingwa mara 11 wa Kombe la FKF na moja ya timu zilizotwaa mataji mengi nchini, inajiandaa kwa mechi ya raundi ya 32 ya Kombe la Mozzart Bet dhidi ya Dero FC itakayochezwa hapo kesho katika uwanja wa Mamboleo, Kaunti ya Kisumu.
K’Ogalo wanaingia kwenye mechi hiyo wakiwa na nia ya kufuta kumbukumbu ya kichapo cha kushtukiza cha mabao 2–1 dhidi ya Nairobi United, timu iliyopanda daraja hivi karibuni, katika fainali ya Kombe la FKF msimu wa 2024/2025 iliyochezwa katika Uwanja wa Ulinzi Sports Complex.
Kipigo hicho kilimaliza msimu bila taji kwa Gor Mahia, hali ambayo ni nadra kwa klabu hiyo yenye historia ndefu ya kutawala soka la humu nchini, na sasa wanatafuta kurejea katika njia ya ushindi kwa kutwaa kombe hilo.
Imetayarishwa na Cyrus Sifuna
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































