WAMALWA AZUNGUMZIA VIFO KITENGELA
Kiongozi wa Chama cha DAP Kenya, Eugene Wamalwa, amesema watu wawili walifariki na takribani Wakenya 50 kujeruhiwa wakati wa mkutano wa Linda Mwananchi uliofanyika Kitengela.
Akizungumza katika mkutano na wanahabari Wamalwa ameeleza masikitiko yake na kudai kuwa kulikuwa na matumizi ya nguvu kupita kiasi.
Aidha, ametoa wito kwa jumuiya ya kimataifa kuingilia kati akisema kuna ongezeko la ukatili wa polisi katika mazingira ya kisiasa yanayoendelea kuwa tete.
Imetayarishwa na Cyrus Sifuna
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































