#Local News

NTSA KUTUMIA KAMERA MAALUM KUDUMISHA SHERIA BARABARANI

Rais William Ruto ameiagiza Mamlaka ya Kitaifa ya Uchukuzi na Usalama (NTSA), pamoja na Wizara ya Uchukuzi, kutekeleza mifumo ya kutumia kamera maalum za trafiki kuwanasa wanaovunja sheria katika barabara mbalimbali nchini.

Akihutubia Baraza la Kitaifa la Utawala wa Haki kwenye Ikulu ya Nairobi Ruto amemkabili Waziri wa Uchukuzi Davis Chirchir na Mkurugenzi Mkuu mpya wa NTSA Nashon Kondiwa kuhusu maendeleo ya polepole katika utekelezaji wa mfumo huo ambao unatarajiwa kutoza faini za papo hapo.

Mpango huo unalenga kuimarisha usalama barabarani, kuboresha usimamizi wa trafiki, na kuimarisha utekelezaji wa kanuni za trafiki nchini kote.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *