#Business

KENYA YAANGAZIA MAUZO YA KWENDA CHINA KWA KASI KABLA YA KUONDOLEWA USHURU

Matarajio yanaongezeka kote katika sekta ya kilimo ya nje ya Kenya huku Uchina inapojitayarisha kutekeleza sera ya kutotoza ushuru kwa bidhaa mbalimbali za Afrika kuanzia Mei 1.

Kwa wengi, hiyo ni hatua isiyokuwa ya kawaida ambayo wauzaji bidhaa nje wanasema inaweza kufafanua upya mtiririko wa biashara kati ya bara na uchumi wa pili kwa ukubwa duniani. Sio tu juu ya gharama za chini, ni juu ya ufikiaji wa msingi mkubwa wa watumiaji.

Mwezi jana Kenya iliripoti shehena yake ya kwanza ya bidhaa kwa China chini ya mpango wa kutotoza ushuru. Shehena hiyo, ambayo inajumuisha jumla ya makontena 54 ya parachichi, mafuta ya parachichi, kahawa na maharagwe mabichi, iliondoka kutoka mjini Nairobi hadi Bandari ya Mombasa kwa ajili ya kusafirishwa hadi China, kulingana na Wizara ya Uwekezaji, Biashara na Viwanda ya Kenya.

Imetayarishwa na Maurine Amwayi

KENYA YAANGAZIA MAUZO YA KWENDA CHINA KWA KASI KABLA YA KUONDOLEWA USHURU

NAIROBI KUPATA SURA MPYA 

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *