#Athletics #Sports

JEPCHIRCHIR AJIONDOA MBIO ZA LONDON

Bingwa wa dunia wa mbio za marathon Peres Jepchirchir amejiondoa katika mashindano ya London Marathon yanayotarajiwa kufanyika Aprili 26 kutokana na majeraha aliyopata mwezi Desemba.

Kujiondoa kwake kunafuatia pia hatua ya Sifan Hassan ambaye naye amejiondoa, hali inayopunguza ushindani mkali uliotarajiwa katika mbio hizo.

Waandaaji wamesema Jepchirchir amekuwa akisumbuliwa na jeraha tangu alipochuana katika mbio za Valencia, ambapo alimaliza wa pili nyuma ya Joyciline Jepkosgei.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *