#uncategorized

MBIO ZA UBINGWA ZAZIDI KUPAMBA MOTO LIGI KUU

Mbio za ubingwa wa ligi kuu ya Kenya zinaingia hatua muhimu mwishoni mwa wiki hii huku mechi za ushindani mkali zikitarajiwa kuamua mwelekeo wa msimamo wa ligi

AFC Leopards watachuana na mabingwa watetezi Kenya Police huku Gor Mahia wakipambana na Bandari walio katika kiwango kizuri hali inayoongeza presha kwa timu zinazowania ubingwa

Ushindi wa hivi karibuni wa Tusker dhidi ya Gor Mahia umefanya ushindani kuwa mkali zaidi huku tofauti ya alama ikiwa ndogo na kila timu ikihitaji ushindi ili kuendelea kuwa kwenye mbio za kutwaa taji la ligi kuu.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *