#uncategorized

SHUJAA WAANGUKIA AUSTRALIA KWENYE MECHI YA UFUNGUZI

Timu ya taifa ya raga ya wachezaji saba Shujaa imeanza kampeni yake ya Hong Kong kwa kichapo cha alama kumi na nne kwa tano dhidi ya Australia katika mechi ya Kundi C iliyoonyesha mapungufu ya ulinzi pamoja na dalili za matumaini

Australia walianza kwa kasi wakipata majaribio mawili ya haraka kupitia Josh Turner na James Turner huku makosa ya nafasi katika safu ya ulinzi ya Shujaa yakigharimu timu hiyo na kuwapa wapinzani uongozi wa alama kumi na nne bila majibu kipindi cha kwanza

Shujaa walipata nafasi nzuri kupitia Patrick Odongo aliyefika kwenye mstari wa majaribio lakini juhudi hiyo ilikataliwa baada ya mapitio kuonyesha kosa katika maandalizi ya shambulizi hali iliyozima matumaini ya kurejea mapema katika mchezo huo.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *