#uncategorized

WAWAKILISHI WADI NYAMIRA WASHINIKIZA NYONGEZA YA MGAO WA KAUNTI

Mwenyekiti wa kamati ya bajeti katika bunge la kaunti ya Nyamira George Abuga amewaongoza wawakilishi wadi kwenye kaunti hiyo kushinikiza nyongeza ya mgao kwa kaunti ili kufanikisha miradi ya maendeleo.

Viongozi hao wamesema kucheleweshwa kwa mgao huo ambao pia wanasema hautoshi, kumefanya kaunti nyingi kusalia nyuma kimaendeleo.

Tayari bunge la kitaifa limetupilia mbali pendekezo la seneti kuongeza mgao wa kaunti.

Imetayarishwa na: Antony Nyongesa

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *