KUSHUTUMU URUSI NI UNAFIKI, GAVANA NASSIR
Siku moja baada ya rais William Ruto kulishutumu taifa la Urusi kuvamia Ukraine, gavana wa Mombasa Abdulswammad Nassir ameshtumu hatua hiyo akiitaja kuwa unafiki.
Kulingana na gavana huyo, msimamo wa rais Ruto unaoegemea upande mmoja, akizingatiwa kwamba kuna mapigano yanayoendelea katika mataifa mengine.
Aidha, amewataka wabunge kutilia maanani maslahi ya wananchi wakati wa kupitisha mswada wa kifedha wa mwaka 2024-25
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































