MAAFISA WAKUU WAKAMATWA KWA MADAI YA ULAGHAI KATIKA AFISI YA MUDAVADI
Ofisi ya Waziri mwenye mamlaka makuu na Wizara ya Mambo ya Nje Musalia Mudavadi imethibitisha kukamatwa kwa baadhi ya viongozi waandamizi katika wizara hiyo.
Katika taarifa, uchunguzi uliofanywa siku ya Jumamosi ulisababisha kukamatwa kwa watu hao kwa madai ya kusaidia walaghai ambao wanasemekana kuwalaghai wageni katika afisi ya Mudavadi.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo ililenga kuvuruga vitendo vinavyoripotiwa vya matumizi mabaya ya afisi kwa watu wanaodaiwa kuwa ni matapeli.
Imetayarishwa na Janice Marete
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































