MNYAMA ASIYEFAHAMIKA ALETA JOTO LIKUYANI
Wakazi wa Kijiji cha Lugulu eneo bunge la Likuyani kaunti ya Kakamega wanaishi kwa hofu kutokana na madai kwamba wamemwona mnyama asiyefahamika ikivamia mifugo wao.
Wakizungumza na wanahabari, wakazi hao wamesema kwamba hofu hiyo imeathiri masomo huku wakihofia usalama wa wanao wanapoelekea shuleni.
Aidha, wameitaka idara ya wanyamapori nchini KWS kuingilia kati na kumnasa mnyama huyo.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 





















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































