KENYA YAONGEZA MEDALI AFRICAN YOUTH GAMES

Idadi ya medali za Kenya katika mashindano yanayoendelea ya wanamichezo wa umri wa kati ya miaka 14-17 African Youth Games nchini Angola imeendelea kupanda, baada ya timu ya riadha kutia fora kwa kushinda medali mbali mbali. Wesley Kiplagat alishinda nishani ya fedha katika mbio za mita 3,000 kwa wavulana, akiandikisha muda wa dakika 8, sekunde […]

KCB YAKATA NYORORO ZA PRISONS

Klabu ya voliboli ya KCB ilijiimarisha na kuvuna ushindi wa seti 3-0 dhidi ya Nairobi Prisons kwenye ligi ya wanawake ya shirikisho la voliboli KVF uwanjani Nyayo jijini Nairobi. Vipusa hao wa benki walikata nyororo za magereza kwa seti 2 za 25-19 na 25-21, kocha mkuu Japheth Munala akiwaondoa wachezaji mahiri baada ya kuweka msingi […]

MASWALI KUHUSU KIFO CHA JIRONGO

Familia ya mfanyabiashara na mwanasiasa tajika Cyrus Jirongo, imeshinikiza majibu kuhusu utata unaozingira kifo cha mfanyabiashara huyo kwenye ajali siku ya Ijumaa usiku, polisi wakisema Jirongo alikuwa akielekea Nairobi kwenye gari lake wakati wa ajali hiyo. Hata hivyo, kulingana na mwenyekiti wa kamati ya mipango ya mazishi Fred Gumo na aliyekuwa seneta wa Vihiga George […]

PVK YAKOSOA SERA TATA YA MAKANISA

Muungano wa Pentecostal Voice of Kenya PVK umeitaka serikali kusitisha mchakato wa kubuniwa kwa sera ya kudhibiti mashirika ya kidini, kufuatia kuondolewa kwa mswada wa kudhibiti mashirika hayo wa mwaka 2024. Ikiongozwa na mwenyekiti wake Apostle Peter Manyuru ambaye pia ni kiongozi wa kanisa la JTM, PVK imehofia kwamba sera hiyo itayanyima makanisa na mashirika […]

WATU 10 WAFARIKI KWENYE AJALI HOMA BAY

Watu 10 wamefariki kwenye ajali ya barabarani katika kituo cha kibiashara cha Chabera kaunti ya Homa Bay huku wengine 6 wakiachwa na majeraha mabaya usiku wa kuamkia leo, baada ya matatu walimokuwa wakisafiria kugongana ana kwa ana na lori. Imeafiriwa kuwa waathiriwa walikuwa wakitoka kwenye hafla ya harusi katika kaunti ya Kakamega, naibu chifu wa […]

RUTO KUONGOZA KIKAO NA MAWAZIRI

Hazina ya kitaifa ya miundomsingi itabuniwa rasmi hii leo kwenye kikao cha baraza la mawaziri kitakachoongozwa na Rais William Ruto, ambaye ameendelea kuitetea hazina hiyo licha ya pingamizi. Kwa mujibu wa Ruto, Kenya itakuwa miongoni mwa mataifa yaliyostawi kiuchumi mfano wa Singapore kupitia fedha zitakazokusanywa kupitia hazina hiyo. Hata hivyo, kinara wa Wiper Kalonzo Musyoka, […]

Онлайн‑слоты в Казахстане: как они растут Летом в Алматы, когда жара не даёт выйти на улицу, а зимой в Астане холодок обхватывает всё, многие ищут способ расслабиться дома.Онлайн‑казино отвечают на этот запрос, предлагая разнообразные игры, удобный интерфейс и быстрые выплаты.В 2024‑м году одной из самых заметных платформ стал Slottica.kz, который позиционирует себя как “премиальный” сервис […]

HAKIMI AJUMUISHWA KIKOSINI MOROCCO LICHA YA JERAHA

Timu ya taifa ya soka ya Morocco imemjumuisha nahodha Achraf Hakimi katika kikosi cha wahezaji 26 wataowakilisha taifa hilo katika kipute cha taifa bingwa barani Africa AFCON kitakachoandaliwa nchini humo wiki ijayo. Beki huyo mwenye umri wa miaka 27, aliumia muundi wa mguu kwenye mechi kati ya klabu yake ya PSG na Bayern Munchen mwezi […]

KPL YAENDELEA HUKU KCB FC IKIPANDA

Ligi kuu ya soka KPL inaendelea hii leo ambapo mechi kadhaa zimeratibiwa kuchezwa katika nyuga mbali mbali. APS Bomet watakuwa wenyeji wa Posta Rangers, Bidco United waialike Mathare United, Kakamega Homeboyz dhidi ya Shabana huku Nairobi United wakilenga kujifufua watakapokutana na Murang’a Seal. Pambano kali litakuwa kati ya Bandari na Gor Mahia, Gor wakilenga kuondoa […]

KENYA YAPATA MEDALI ZA KWANZA ANGOLA

Kikosi cha Kenya katika michezo ya vijana kimepata medali za kwanza katika mashindano yanayoendelea nchini Angola ya 2025 African Youth Games kwa kujizolea nishani 2 za shaba katika siku ya kwanza. Timu ya Carter ilikuwa ya kwanza kunyakua nishani yake, na kuweka msingi kwa nishani zaidi kwa taifa kwenye mashindano hayo kabla ya Margaret Nyevu […]