#Business

GHARAMA YA MAFUTA: IMF YAONYA HALI YA UCHUMI WA KENYA

Shirika la fedha duniani (IMF) limerekebisha mtazamo wake wa kiuchumi kwa mataifa ya kusini mwa Jangwa la Sahara kushuka, ikiwa ni pamoja na makadirio ya Kenya, kufuatia kupanda kwa bei ya mafuta hivi majuzi ambayo inaangazia kudorora kwa uchumi.

Katika mtazamo wake wa hivi punde wa uchumi wa Kikanda wa Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara, IMF imebainisha kuwa ingawa kanda hiyo ilipata kasi ya ukuaji wa asilimia 4.5 mwaka 2025, kiwango cha juu zaidi katika miaka kumi, kasi hiyo inatarajiwa kupungua hadi asilimia 4.3 mwaka 2026.

Kupungua huko kwa kiasi kikubwa kunahusishwa na mzozo unaozidi kuongezeka katika Mashariki ya Kati, ambao mienendo yake ya kiuchumi duniani inaongeza gharama na kufifisha matarajio ya ukuaji katika uchumi wa Afrika.

Kama nchi inayoagiza mafuta, Kenya iko katika kundi la mataifa ambayo IMF inaonya kuwa itabeba mzigo mzito zaidi, ikikabiliwa na kuzorota kwa usawa wa biashara na gharama ya juu ya maisha.

Imetayarishwa na Maurine Amwayi

GHARAMA YA MAFUTA: IMF YAONYA HALI YA UCHUMI WA KENYA

BRIGHTON YAIDUWAZA CHELSEA EPL

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *