SIKU YA MAANDAMANO HII HAPA
Maandamano yameratibiwa kufanyika katika maeneo mbali mbali ya nchi hii leo ambapo waandalizi wanalalamikia bei ya juu ya mafuta iliyotangazwa wiki jana na serikali.
Kupitia kauli mbiu ya Reject Fuel Prices, wakenya wanalenga kuishinikiza serikali kupunguza bei ya mafuta mbali na kuangazia gharama ya juu ya maisha ambayo imechangiwa na ongezeko la bei hizo.
Jijini Nairobi, kamanda wa polisi Issa Mohamoud ameshikilia kuwa maandamano hayo ni haramu.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 










































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































