GACHAGUA: MAANDAMANO YA MAFUTA BADO JUMANNE
Muungano wa upinzani nchini umesisitiza kuwa maandamano ya kitaifa yalioratibiwa kufanyika hapo kesho kuishinikiza serikali kupunguza bei ya mafuta yangalipo.
Ukiongozwa na kinara wa chama cha DCP Rigathi Gachagua, muungano huo umesema lengo la maandamano hayo ni kulalamikia gharama ya juu ya maisha itakayochangiwa na bei mpya za juu za mafuta.
Aidha, amewahimiza vijana kusajiliwa kama wapiga kura.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 










































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































