MWANAMME ADAIWA KUMWUA MWANAWE KWA UPANGA
Polisi katika kaunti ya Kakamega wanaendeleza uchunguzi katika tukio ambapo mwanamme mmoja katika Kijiji cha Emabusi eneo bunge la Ikolomani, ameripotiwa kumuua mwanawe kwa kumkatakata na kuwajeruhi wengine vibaya.
Mwanamme huyo aliyeshambuliwa na wananchi wakati wa tukio hilo, anatibiwa hospitalini chini ya ulinzi mkali, huku walioshuhudia tukio hilo wkaisema alichukua hatua hiyo kutokana na mzozo wa kinyumbani na mkewe.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 










































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































