WATU KADHAA WAKAMATWA KATIKA MAANDAMANO YA MAFUTA NAIROBI
Takriban watu kumi na mmoja wamekamatwa baada ya kujaribu kuandamana jijini Nairobi kupinga kupanda kwa bei ya mafuta
Polisi wa kutuliza ghasia waliwatawanya waandamanaji hao walipokuwa wakijaribu kuelekea katikati ya jiji kutoka eneo la Archives na kuwapeleka katika kituo cha polisi cha Central
Kamanda wa polisi wa Nairobi Issa Mohamud amesema maafisa walikuwa wakishirikiana na kundi hilo kudumisha utulivu akiongeza kuwa hali ya jiji ilikuwa tulivu kwa sehemu kubwa ya asubuhi
Imetayarishwa na Cyrus Sifuna
English 










































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































