#Local News

WATU KADHAA WAKAMATWA KATIKA MAANDAMANO YA MAFUTA NAIROBI

Takriban watu kumi na mmoja wamekamatwa baada ya kujaribu kuandamana jijini Nairobi kupinga kupanda kwa bei ya mafuta

Polisi wa kutuliza ghasia waliwatawanya waandamanaji hao walipokuwa wakijaribu kuelekea katikati ya jiji kutoka eneo la Archives na kuwapeleka katika kituo cha polisi cha Central

Kamanda wa polisi wa Nairobi Issa Mohamud amesema maafisa walikuwa wakishirikiana na kundi hilo kudumisha utulivu akiongeza kuwa hali ya jiji ilikuwa tulivu kwa sehemu kubwa ya asubuhi

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *