TANZANIA YAMKOSOA RUTO KWA ‘KUWADOGOSHA’ MAJIRANI
Serikali ya Tanzania imepuzilia mbali kauli za Rais William Ruto kwamba Kenya ina barabara nyingi za lami ikilinganishwa na mataifa yote katika Jumuiya ya Afrika Mashariki, ikisema kauli hizo ni za kudhalilisha.
Akitetea bei za juu za mafuta nchini ikilinganishwa na mataifa jirani, Ruto alisema kuwa Kenya ni nchi yenye kiwango cha kati cha uchumi, na kwamba majirani zake ni wa kiwango cha chini.
Hata hivyo, Waziri wa ujenzi wa Tanzania Abdallah Ulenga, amesema kauli hizo si sahihi.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 










































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































