#Local News

MURKOMEN: KUNA MAELFU YA WAHUNI NCHINI

Imebainika kwamba kuna magenge 100 yenye maelfu ya wanachama ambayo yanaendelea kuvuruga mikutano ya kisiasa nchini, serikali ikidai magenge hayo yanafadhiliwa na baadhi ya wanasiasa.

Akiwa mbele ya kamati ya bunge kuhusu usalama, Waziri wa usalama wa kitaifa Kipchumba Murkomen, ameilaumu idara ya mahakama kutokana na ongezeko la uhuni, akisema idara hiyo imelegeza masharti.

Aidha, amesema washukiwa 14 kati ya 17 waliomshambulia seneta wa Vihiga Godfrey Osotsi walitorokea nchi jirani na wanasakwa.

Imetayarishwa na Antony Nyongesa

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *