SERIKALI YATOA FEDHA ZA UFADHILI KWA MUHULA WA PILI
Serikali imetoa shilingi bilioni ishirini na tatu nukta nne za ufadhili kwa shule za umma kabla ya kufunguliwa kwa muhula wa pili Jumatatu ili kuhakikisha shughuli za masomo zinaendelea bila usumbufu
Katibu Mkuu wa Elimu ya Msingi Julius Bitok amesema fedha hizo zitaingia katika akaunti za shule kufikia Ijumaa ili kuwapa wasimamizi muda wa kujiandaa ipasavyo kwa ufunguzi wa shule
Ameongeza kuwa serikali pia inaweka kipaumbele katika usambazaji wa vifaa vya kujifunzia ikiwemo vitabu vya darasa la kumi kama sehemu ya utekelezaji wa mfumo mpya wa elimu unaolenga kuimarisha ujuzi wa wanafunzi.
Imetayarishwa na Cyrus Sifuna
English 










































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































