WIZARA YA AFYA YAONYA KUHUSU MLIPUKO WA MAGONJWA KISA TAKATAKA
Wizara ya afya imesema kuwa wakenya wengi wako katika hatari ya maambukizi ya magonjwa kutokana na ongezeko la taka zinazotupwa ovyo ovyo.
Katibu mkuu katika wizara ya afya Mary Muthoni amesema kuwa kwa sasa wakenya hasa walio katika maeneo ya miji ndio walio katika hatari kubwa ya mlipuko wa magonjwa hayo.
Aidha takwimu zimeonyesha kuwa kenya huzalisha takriban tani elfu 22 kwa siku huku asilimia kumi zikiwa ndizo zinazosimamiwa ipasavyo.
Imetayarishwa na Cyrus Sifuna
English 










































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































