#Local News

UPINZANI WATISHIA KUMREJESHA RAIS RUTO ICC

Hulka ya matumizi ya magenge ya wahuni kuvuruga mikutano ya kisiasa imechukua mkondo mpya, muungano wa upinzani sasa ukitishia kuishtaki serikali ya Rais William Ruto katika mahakama ya kimataifa kuhusu uhalifu, ICC.

Viongozi wa muungano huo akiwemo Kalonzo Musyoka wa Wiper na Rigathi Gachagua wa DCP, wamedai kuwa magenge hayo yanafanya kazi kwa ushirikiano na idara ya polisi kutatiza mikutano ya wanaopinga serikali.

Wameilaumu wizara ya usalama wa ndani kwa kutokana na hulka hiyo.

Imetayarishwa na Antony Nyongesa

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *