MAFURIKO YAZUA HOFU NAKURU
Hofu ingali imetanda katika eneo la Kaptembwo kaunti ya Nakuru baada ya mtu mmoja kufariki na makumi ya familia kuachwa bila makao kufuatia mafuriko yaliyotokana na mvua kubwa.
Sammy Tarus amepoteza uhai baada ya kusombwa na mafuriko kwenye barabara kuu ya Nakuru kuelekea Eldoret, vidimbwi sasa vikiwa vimeanza kuchimbika kando kando mwa barabara hiyo na kuzua hofu ya maporomoko.
Mwili wake umeopolewa mapema leo na kupelekwa katika hifadhi ya hospitali ya Nakuru.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 










































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































