MPOX YAZIDI KUENEA

Unatakiwa kuchukua tahadhari kujilinda dhidi ya ugonjwa wa Mpox.Tayari visa 137 vimeripotiwa katika kaunti 17 nchini. Katibu katika wizara ya afya Mary Muthoni anasema sampuli 597 zimefanyiwa vipimo katika mahabara ya kitaifa. Watu wengine 400 waliokuwa karibu na waathiriwa wametambuliwa na 15 kati yao wamepatikana na virusi vya Mpox. Imetayarishwa na Maureen Amakhobe

JAJI MUSTAAFU MUTUNGA NA KARUA WASHTAKI TANZANIA

Kuna haja ya wapatanishi kuingilia kati na kuondoa uhasama uliopo kati ya wanaharakati wa humu nchini na serikali ya tanzania. Hii ni baada ya aliyekuwa jaji mkuu Willy Mutunga na mwanasiasa Martha Karua kuwasilisha kesi Katika mahakama ya haki ya afrika mashariki dhidi ya serikali hiyo kwa kosa la kuwazuilia kinyume na sheria na kuwazuia […]

WATALII 5 WAFA KWENYE AJALI NYANDARUA

Watalii 5 wenye asili ya Kihindi wamethibitishwa kufariki huku wengine kadhaa wakijeruhiwa kwenye ajali ya baada ya basi dogo walimokuwa wakisafiria kuanguka katika eneo la Gichaka, kwenye barabara ya Nakuru kuelekea Ol-Joro Ork kaunti ya Nyandarua. Imearifiwa kuwa watalii hao walikuwa wakisafiri kutoka mbuga ya Wanyama ya Maasai Mara kabla ya breki za basi hilo […]

RUTO: TUNAKULA MATUNDA YA ‘MAAMUZI MAGUMU’

Tunavuna matunda ya maamuzi magumu na yenye manufaa kwa taifa ambayo sasa yamechangia kuimarika kwa uchumi wa nchi. Ndiyo kauli ya Rais William Ruto, akizungumza kwenye kikao na wasanii katika Ikulu ya Nairobi. Rais amesisitiza kwamba hakuna muda ambao umepotea katika siku zake 1,000 mamlakani, akisema kila siku imekuwa ni kuchapa kazi. Imetayarishwa na Antony […]

MBIOMBIO ZA KUSAJILI WACHEZAJI

Vilabu vya Ligi Kuu ya Uingereza viko kwenye kinyang’anyiro dhidi ya masaa moja ili kupata mikataba iliyokamilika kabla ya dirisha la usajili la majira ya kiangazi litakapofungwa Jumanne. Liverpool bado wako kwenye mazungumzo ya kuwasajili nyota wa Bayer Leverkusen, Florian Wirtz na beki wa Bournemouth Milos Kerkez, huku Chelsea pia wakisukumana kwa pande tatu tofauti […]

AFCON YAKABILIWA NA MKANGANYIKO

Maandalizi ya Kenya kwa Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2027 yamekabiliwa na mkanganyiko mkubwa baada ya ufinyu wa bajeti kwa idara ya michezo, huku kukiwa na kupunguzwa kwa ufadhili katika idara hiyo. Makadirio ya bajeti yaliyopendekezwa kwa mwaka wa kifedha wa 2025-2026 yaliyowasilishwa bungeni wiki hii, yanaonyesha kupunguzwa kwa Ksh.1.1 bilioni kwa Idara ya […]

SIMBA WAANZA KWA MNGURUMO KULE CAPE TOWN

Simbas wa Kenya walifanya vyema katika kipindi cha kwanza lakini hawakuweza kuvumilia walipolazwa 24-42 na Junior Springboks katika mechi yao ya pili ya kirafiki ya maandalizi ya msimu mpya wa ziara ya Afrika Kusini Jumatatu alasiri mjini Stellenbosch, Cape Town. Wakiwa wametoka sare ya 17-17 na SWD Eagles katika mechi yao ya ufunguzi, Simbas waliingia […]

UCHUNGUZI WA FIGO WATUA ELDORET

Serikali inaendeleza juhudi za kutegua kitendawili cha upandikizaji wa viungo vya mwili ikiwemo figo na madai ya ulanguzi wa viungo hivyo katika hospitali ya kibinafsi ya Mediheal, tayari malalamishi ya wananchi yakianza kupokelewa jijini Eldoret. Mwenyekiti wa kamati inayochunguza huduma za upandikizaji huo profesa Elizabeth Bukusi, amewataka wakazi walio na malalamishi kuhusu huduma hizo katika […]

DIG LANGAT KIKAANGONI

Familia ya mwanablogu Albert Ojwang aliyefariki mikononi ma maafisa wa polisi baada ya kukamatwa imeendelea kudai haki ya mwanao, ikiwalaumu polisi kutokana na kifo hicho. Ikiongozwa na Meshack Ojwang ambaye ni babake kijana huyo, familia hiyo imetilia shaka uwazi kwenye uchunguzi wa kifo hicho, kauli sawa ikishikiliwa na wanaharakati wanaoshinikiza kujiuzulu kwa naibu inspekta mkuu […]

MASWALI KUHUSU KIFO CHA OJWANG’

Huku upasuaji wa maiti ya Albert Ojwang, mwanablogu aliyekamatwa na kufariki akiwa kwenye seli za polisi kwa madai ya kumchafulia jina naibu inspekta mkuu wa polisi Eliud Langat ukitarajiwa hii leo, maswali yameendelea kuibuliwa kuhusiana na kukamatwa kwake. Viongozi wanaoegemea chama cha ODM wametaka kujua ni kwanini kijana huyo akasafirishwa kutoka Homa Bay hadi Nairobi, […]