HARRIET OKACH ATEULIWA KUA MWENYEKITI WA KRU

Harriet Okach ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Chama cha Raga nchini (KRU), na kuwa mwanamke wa kwanza kabisa kushikilia wadhifa huo katika historia ya shirikisho hilo. Uteuzi wake ulithibitishwa Alhamisi, kufuatia kujiuzulu kwa Alexander ‘Sasha’ Mutai wiki jana. Katika hotuba yake ya kwanza baada ya uteuzi huo, Okach aliahidi kuwaleta washikadau wote pamoja kwa ajili ya […]

KAULI YA VIONGOZI WA KALENJIN TRANS NZOIA

Viongozi wa jamii ya Kalenjin katika kaunti ya Trans Nzoia wameikosoa serikali kwa madai ya kumhangaisha kisiasa gavana wa kaunti hiyo George Natembeya na maafisa wengine wa serikali yake waliokamatwa na kufunguliwa mashtaka. Wakiongozwa na Eliud Tormoi, viongozi hao wamesema serikali inalenga kumdhalilisha gavana huyo, wakitoa wito kwa taasisi za serikali kutekeleza majukumu yao bila […]

AJIRA YA CLIMATE WORX

Zaidi ya vijana 100,000 katika kaunti 46 nchini watanufaika na mpango wa kazi mtaani chini ya mpango wa Climate Worx uliozinduliwa na serikali ili kutoa nafasi za ajira kwa vijana. Katibu katika wizara ya usalama Raymond Omolo na mwenzake wa makaazi Charles Hinga, wamesema usajili wa watakaojiunga na mradi huo unatarajiwa kuanza rasmi katika muda […]

ULANGUZI WA FIGO: MBUNGE ADAI DCI INAMTISHIA

Mbunge wa Nandi Hills Bernard Kitur amedai kwamba Maisha yake yako hatarini baada yake kufichua mtandao wa kimataifa unaojihusisha na ulanguzi wa viungo vya mwili wa binadamu, anaosema unashirikiana na baadhi ya hospitali na kufanikishwa na maafisa wa usalama. Akizungumza akiwa mbele ya kamati ya afya bungeni kuthibitisha madai kuhusu ulanguzi huo, Kitur amesema kuwa […]

MZIGO WA KARO MLANGONI

Huenda wazazi wakagharamika zaidi katika ulipaji wa karo kutokana na uamuzi wa wizara ya elimu kupunguza mgao wa masomo kwa shilingi bilioni 22 kwenye bajeti ya mwaka wa 2025-26. Akizungumza mbele ya kamati ya elimu bungeni, waziri wa elimu Julius Ogamba, amesema pengo hilo litazibwa na wazazi ili kufadhili elimu katika shule za msingi na […]

SERIKALI INAWALINDA, KINDIKI

Serikali imewahakikishia wakenya usalama licha ya joto la kisiasa linaloendelea kushuhudiwa nchini kuelekea kwenye uchaguzi mkuu ujao. Akizungumza wakati wa hafla ya kuwawezesha akina mama kiuchumi katiika kaunti ya Kitui, Naibu Rais Kithure Kindiki amesema serikali iko macho kuwakabili viongozi wanaowachochea wananchi. Imetayarishwa na Antony Nyongesa

MAKAMANDA KUWAJIBIKIA UFISADI WA MAAFISA WAO

Makamanda wa polisi kote nchini watabebeshwa msalaba wa maafisa fisadi walio chini yao, ikiwa ni njia moja ya idara ya polisi kujisafisha kutokana na tope la ufisadi ambalo limeiandama kwa miaka. Agizo hilo limetolewa na inspekta mkuu wa polisi Douglas Kanja, baada ya kikao na makamanda hao jijini Nairobi, akiwaagiza kuunda kamati za kuzuia ufisadi […]

POLISI KUBUNI KAMATI ZA KUKABILI UFISADI

Wakuu wa usalama wameagizwa kuanzisha kamati maalum za kukabiliana na ufisadi unaohusisha polisi kwenye kaunti kufuatia agizo la inspekta mkuu wa polisi. Akiongea kwenye mkutano na wakuu wa usalama Mkuu wa polisi Douglas Kanja anasema hatua hiyo inachukuliwa kutokana na kukithiri kwa visa vya ufisadi anavyosema pia vinawahusisha wananchi. Imetayarishwa na Maureen Makhobe

KILIMO CHA MIWA KUWAFAIDI WAKULIMA

Wakaazi wa eneo la magharibi na maeneo mengine yanayokuza zao la miwa wataanza kufaidi na zao hilo baada ya rais kuelezea mpango wa kuboresha sekta ya miwa. Akiongea kwenye mkao na wabunge kutoka kaunti za Vihiga Kakamega Bungoma Trans nzoia na Busia rais William ruto anasema wanaekeza katika marekebisho umuhimu ikiwemo kuimarisha usimamizi wa sekta […]

MIGOSI ATAKIWA KUWEKA WAZI MIRADI YA ELIMU

Wizara ya elimu imetakiwa kuorodhesha miradi yote inayoendeshwa katika shule zilizoko maeneo bunge tofauti nchini na ripoti hiyo kuwasilishwa mbele ya kamati ya bunge kuhusu elimu. Waziri wa elimu Julius Migosi akiwa mbele ya kamati ya bunge ametakiwa kuwashirikisha wabunge na wakuu wengine wa elimu katika ujenzi wa miradi katika shule zilizoko katika maeneo bunge […]