IDADI YA WALIOSAJILIWA NA IEBC KUFIKIA SASA
Ni wakenya 90,020 pekee ndio wamesajiliwa kama wapiga kura wapya katika zoezi linaloendeshwa na tume huru ya uchaguzi na mipaka IEBC.
Kwa mujibu wa ripoti ya tume hiyo, kaunti za Nairobi, Kiambu na Machakos zinaongoza kwa idadi ya waliosajiliwa kwa wapiga kura wapya 16,512, 9,917 na 4,026 mtawalia.
Kufikia Oktoba 31, jumla ya wapiga kura 15,619 walikuwa wamehamishia kura zao katika vituo vipya.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 
































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































