#Local News

VIONGOZI WA PWANI WATAKA JOHO KUWA NAIBU RAIS 2027

Baadhi ya wanachama wa chama cha ODM kutoka eneo la Pwani wanaendeleza kampeni za kumtaka Waziri wa Madini, Hassan Joho, kuwa Naibu Rais mwaka 2027.

Wakiongozwa na Naibu Kiongozi wa chama na Gavana wa Mombasa, Abdulswamad Nassir, pamoja na Gavana wa Kilifi Gideon Mung’aro,viongozi hao wameonyesha  imani kuwa chama kitashinda nafasi zote za uongozi.

Nassir amesema kuwa chini ya makubaliano ya serikali jumuishi, ODM itadai nafasi ya Naibu Rais, akimtaja Joho kuwa mgombea anayefaa.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *