RUTO AZINDUA UJENZI WA SOKO LA IKONGE, NYAMIRA

Shughuli za kibiashara katika eneo bunge la Mugirango North kaunti ya Nyamira zinatarajiwa kuimarika katika siku zijazo kufuatia uzinduzi wa ujenzi wa soko la Ikonge huku Rais William Ruto akisema shilingi bilioni 15 zimetengewa ujenzi wa masoko ya kisasa na nyumba za bei nafuu kwenye kaunti hiyo. Akizungumza baada ya kuweka jiwe la msingi la […]

KENYA YAWEKA JUHUDI ZA BIASHARA PASI USHURU NA INDIA

Kenya inalenga kuweka mkataba wa India utakaowezesha uuzaji na uagizaji wa bidhaa baina ya mataifa hayo bila kutozwa ushuru, FTA. Mkuu wa mawaziri Musalia Mudavadi, amesema Nairobi iko tayarisha kutanua uhusiano wake wa kibiashara na New Delhi kupitia mfumo mwafaka. Lengo la Kenya na kuongeza soko la bidhaa zake na vile vile kuangazia ukosefu wa […]

DCI WAPATA MWILI WA MWANAFUNZI ALIYETOWEKA KISUMU

Makachero wa idara ya upelelezi, DCI wamemkamata mshukiwa mkuu wa mauaji ya mwanafunzi wa kike mwenye umri wa miaka 21 wa chuo kimoja jijini Kisumu. Makachero hao wanaamini kuwa Coleman Okoth ndiye aliyepanga ubakaji wa zamu, kuteswa na kisha kutoweka kwa mpenzi wake huyo wa zamani ambaye mwili wake uliokuwa umeharibi8ka umetikana katika msitu wa […]

MGOMO: MATIBABU YALEMAZWA KNH

Huduma za matibabu katika hospitali ya kitaifa ya Kenyatta zimeripotiwa kukwama baada ya wauguzi hospitalini humo kuanza mgomo kuhusiana na masuala mbali mbali. Miongoni mwa malalamishi yao ni madai ya kucheleweshwa kwa mishahara, ukosefu wa malipo ya pensheni na wenzao kuhudumu kwa mkataba kwa muda mrefu bila ajira ya kudumu. Wameapa kutorejea kazini hadi malalamishi […]

CITY WAFAIDI MASAIBU YA ARSENAL, WAILAZA CHELSEA

Manchester City walitumia fursa ya kuteleza kwa Arsenal katika kinyang’anyiro cha kuwania ubingwa wa taji la ligi kuu ya Uingereza, EPL, kwa kuandikisha ushindi mnono wa mabao 3-0 ugenini dhidi ya Chelsea ugani Stamford Bridge. City walibomoa daraja la wenyeji wao kupitia kwa mabeki Nico O’Reily, Marc Guehi na wing’a Jeremy Doku katika kipindi cha […]

JUNIOR STARLETS WAINUA MATUMAINI YA KOMBE LA DUNIA

Kikosi cha timu ya taifa ya wanawake ya soka kwa wachezaji wasiozidi umri wa miaka 17, Junior Starlets, kiliimarisha matumaini yao ya kufuzu dimba la kombe la dunia kufuatia ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Namibia katika mkondo wa kwanza wa mechi za kufuzu mashindano ya FIFA U17 Women World Cup. Wakiwa ugenini, chipukizi hao […]

RUTO ZIARANI ENEO LA GUSII

Ziara ya Rais William Ruto katika kaunti za Kisii na Nyamira inaingia siku ya pili hii leo huku Rais akiratibiwa kuzindua miradi kadhaa ya maendeleo kwenye ziara yake ya siku 4 eneo hilo. Tayari rais amezindua ukarabati na upanuzi wa uwanja wa michezo wa Kisii, akisema tayari mwanakandarasi na fedha zimetengwa kwa shughuli hiyo. Aidha, […]

WAUGUZI KNH KUANZA MGOMO

Huenda huduma za matibabu katika hospitali ya kitaifa ya Kenyatta zikatatizika kuanzia leo kutokana na mgomo wa wauguzi, wanaodai kwamba mishahara yao imecheleweshwa. Katibu mkuu wa muungano wa kitaifa wa wauguzi, Seth Panyako, amelalamikia madai hayo akiongeza kuwa malipo ya uzeeni hayajalipwa na kwamba wauguzi wanahudumu kwa kandarasi bila kupewa ajira ya kudumu zaidi ya […]

METHU ASISITIZA HAJUTII ‘KUMPASHA’ RUTO

Seneta wa Nyandarua John Methu, amekariri kuwa hajutii kauli zake zilizofasiriwa kama za kumkosea heshima Rais William Ruto wiki jana katika hafla ya mazishi kaunti hiyo, akisema alikuwa akitekeleza wajibu wake kikatiba kuhakikisha Rais anatekeleza majukumu yake. Kwenye mahojiano na kituo kimoja cha runinga, Methu amewakosoa wanaodai alimshambulia Rais kwa maneno, na kwamba hakulenga kumkosea […]

UPINZANI: SERIKALI INAWAFADHILI WAHUNI

Viongozi wa muungano wa upinzani wameibua madai kwamba makundi ya wahuni yanapangwa na serikali kwa lengo la kuvuruga mikutano yao, wakionya kuwa huenda makundi hayo yakalitumbukiza taifa kwenye vurugu. Wakiwa kwenye ziara katika kaunti ya Kajiado, viongozi hao wakiongozwa na Rigathi Gachagua wa DCP wamedai kuwa makundi hayo yanafadhiliwa na wizara ya usalama wa kitaifa. […]