KENYA PIPELINE YALENGA KUFUZU HATUA YA MTOANO, KCB YAANZA KAMPENI CAIRO

Timu ya mpira wa wavu ya  Kenya Pipeline inatarajiwa kufuzu hatua ya mtoano iwapo itapata ushindi wa tatu mfululizo katika mechi za awali za mashindano ya vilabu bingwa Afrika kwa wanawake. Pipeline, inayowania taji la bara kwa mara ya kwanza baada ya miaka 20, itashuka dimbani saa kumi na mbili jioni kumenyana na timu ya La Loi […]

ZARIKA AWEKA MBELE LENGO LA MARUDIANO NA KIRSTY HILL

Bondia mkongwe wa Kenya Fatuma Zarika ameelekeza macho yake katika kutafuta pambano la marudiano na Kirsty Hill huku akiingia katika hatua ya mwisho ya taaluma yake ya ngumi. Bondia huyo mwenye umri wa miaka 41 anatafuta nafasi nyingine ya kupigania taji la Ndondi la Jumuiya ya Madola katika uzani wa Super Featherweight, ambalo alipoteza kwa Hill […]

CHAMA CHA WAMILIKI WA MATATU KIMETHIBITISHA MPANGO WA KUONGEZA NAULI

Rais wa Chama cha Wamiliki wa Matatu Albert Karakacha ametangaza kuwa bei za nauli za magari ya uchukuzi wa umma zitaongezeka kuanzia leo hii. Akizungumza wakati wa mahojiano na kituo kimoja nchini, Karakacha amesema wasafiri kote nchini wanapaswa kugharamia usafiri baada ya wahudumu wa matatu kutangaza mipango ya kuongeza nauli kufuatia ongezeko la hivi punde la bei ya mafuta. […]

UCL: LIVERPOOL, BARCA WABANDULIWA, ARSENAL WAKIJIANDAA

Ousmane Dembele alifunga mara mbili na kuikabidhi timu yake ya Paris St-Germain ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Liverpool na tiketi ya kufuzu kwa awamu ya nusu fainali ya dimba la klabu bingwa bara Ulaya. Ushindi huo uliipa Liverpool kichapo cha jumla ya mabao 4 bila jibu, na kuwabandua nje ya mashindano hayo katika awamu […]

K’OGALO YAONYA KUWA KUTELEZA SI KUANGUKA

Kocha mkuu wa Gor Mahia Charles Akonnor ametoa onyo kwa washindani wao wa taji la ligi kuu ya soka nchini, KPL, dhidi ya kusherehekea kichapo cha Gor Mahia akikariri kuwa mabingwa hao mara 21 wangali katika nafasi nzuri ya kunyakua taji hilo msimu huu. Kauli yake imejiri baada ya Gor Mahia kupoteza nafasi nyingi za […]

AFCON 2027: KENYA, UGANDA NA TANZANIA KUZINDUA MWONGOZO

Mataifa ya Kenya, Uganda na Tanzania yatazindua mwongozo utakaofuatwa katika kuandaa dimba la mataifa bingwa barani Afrika mwaka ujao, AFCON 2027 litakaloandaliwa katika mataifa hayo. Waziri wa michezo Salim Mvurya, amesema mkutano kuhusu uzinduzi huo uliopewa jina la Pamoja Summit, utawaleta pamoja mawaziri Alhamisi wiki ijayo kujadili kuhusu masuala muhimu ikiwemo utoaji wa visa za […]

WAUGUZI, WAKUNGA KNH WASITISHA MGOMO

Utoaji wa huduma za matibabu katika hospitali ya kitaifa ya Kenyatta umerejelea hali ya kawaida baada ya wauguzi kusitisha mgomo wao kufuatia mazungumzo kati ya usimamizi wa hospitali hiyo na muungano wa wauguzi na wakunga. Akitoa tangazo hilo, Waziri wa afya Aden Duale amesema mkataba huo uliafikiwa baada ya pande husika kujitolea kwa mazungumzo ya […]

WIZARA YA KAWI ILIJUA MAFUTA GHUSHI, SENETI YAAMBIWA

Imeibuka kwamba serikali ilikuwa na ufahamu kuhusu uagizaji wa mafuta tata tangu hatua za mwanzo, kabla ya mafuta hayo kuamrishwa kuondolewa nchini kwa kukosa kukidhi viwango na kulisababishia taifa hasara ya mabilioni ya pesa. Akiwa mbele ya seneti, meneja mkuu wa kampuni ya Oryx Kenya Limited Angeline Maangi, amesema kampuni hiyo ilipata ombi la haraka […]

SERIKALI YATAKIWA KUPUNGUZA BEI YA MAFUTA

Serikali imeshinikizwa kuweka mikakati mwafaka ili kuwalinda wakenya dhidi ya gharama ya juu ya maisha kwa kuhakikisha kuwa inapunguza bei ya mafuta licha ya shinikizo katika soko la kimataifa. Katika kikao na wanahabari, mbunge wa Kiharu Ndindi Nyoro ambaye amekuwa mkosoaji wa serikali kuhusu mzigo wa ushuru, ameitaka serikali kuweka ruzuku mbali na kupunguza ushuru […]

PETROLI, DISELI YAVUKA SH.200 KWA LITA

Wakenya sasa watalazimika kuingia mfukoni zaidi kugharamia mahitaji ya kila siku kama vile chakula na usafiri, baada ya serikali kupandisha bei ya petroli kwa shilingi 28.69 kwa lita na diseli kwa shilingi 40.30, bei hiyo ikitekelezwa kwa kipindi cha tarehe 15 Aprili na tarehe 14 mwezi ujao. Kulingana na taarifa ya mamlaka ya kudhibiti kawi […]