ZICO AREJEA POSTA RANGERS

Kocha mkongwe Zedekiah Otieno ametambulishwa rasmi kama kocha mkuu wa Posta Rangers katika uwanja wa Chuo cha Ualimu cha Thogoto. Otieno, anayejulikana kama “Zico,” amejiunga na timu hiyo katika kipindi ambacho imekuwa ikipambana na ukosefu wa uthabiti licha ya kuanza vyema msimu. Kwa uzoefu wa zaidi ya miaka ishirini, akiwa amewahi kuzifundisha timu kadhaa ikiwemo Gor Mahia […]

MSICHANA WA MIAKA 13 APATIKANA AMEFARIKI MAU SUMMIT

Wakazi wa Kijiji cha Casino eneo la Mau Summit wanaomboleza baada ya mwili wa msichana wa miaka 13 kupatikana ndani ya bwawa, tukio linaloshukiwa kuwa mauaji. Msichana huyo aliyetambulika kama Lilian Njambi alionekana mara ya mwisho Jumatatu akicheza na wenzake kabla ya kutoweka jioni, hali iliyosababisha familia na wakazi kuanza msako wa kumtafuta. Mwili wake umepatikana ukiwa na dalili za […]

MWANAUME AFARIKI BAADA YA KUANGUKA KUTOKA JUMBA LA KICC

Mwanaume mmoja amefariki baada ya kuanguka kutoka ghorofa ya juu katika jengo la KICC jijini Nairobi. Kamanda wa polisi eneo la kati Stephene Nyakombo amesema bado hawajabaini chanzo cha tukio hilo wala ghorofa aliyotoka, huku uchunguzi ukiendelea. Mwili wa marehemu umepelekwa katika chumba cha kuhifadhi maiti ukisubiri kutambuliwa na kufanyiwa uchunguzi zaidi, huku polisi wakisema bado wanachunguza iwapo tukio […]

EACC YAJITETEA DHIDI YA UFISADI

Tume ya Maadili na Kupambana na Ufisadi (EACC) imetetea utendakazi wake ikisema imepata mafanikio katika hukumu za kesi na urejeshaji wa fedha za umma zilizoibwa. Mkurugenzi Mkuu Abdi A. Mohamud amesema tume hiyo imefanikiwa kupata asilimia 72 ya hukumu za hatia katika kipindi cha miaka miwili iliyopita na kurejesha shilingi bilioni saba nukta nane za fedha za […]

KAMATI YA BUNGE YACHUNGUZA UHABA WA MAFUTA

Kamati ya Bunge la Taifa kuhusu Kawi na Petroli imezuru maghala ya mafuta ya Kenya Pipeline katika jiji la Nairobi kuchunguza kiini cha uhaba wa mafuta unaoshuhudiwa katika maeneo mbalimbali nchini. Ziara hiyo inalenga kubaini changamoto katika usambazaji na uhifadhi wa mafuta pamoja na hatua zilizochukuliwa kushughulikia hali hiyo. Kamati hiyo imeahidi kuwasilisha ripoti yao baada […]

UN YAZINDUA MRADI WA KUBORESHA MAGEUZI YA KIJANI NCHINI KENYA

Shirika la mazingira la umoja wa mataifa (UNEP) na shirika la makazi la umoja wa mataifa (UN-habitat) yamezindua mradi wenye thamani ya dola za kimarekani milioni 5.2 kubadili mji mkuu wa kenya, nairobi, kuwa kituo cha unyumbukaji wa mabadiliko ya tabianchi, ukuaji chanya wa asili na mfumo wa mzunguko. Ukifadhiliwa na kituo cha mazingira duniani, […]

UCL: YAMAL AKARIRI LIPO TUMAINI DHIDI YA ATLETICO

Mshambulizi wa klabu ya Barcelona Lamine Yamal, amesisitiza kuwa yeye na wachezaji wenza watapigania nembo ya klabu hiyo katika pambano la leo la mkondo wa mwisho wa awamu ya robo fainali katika kombe la klabu bingwa bara Ulaya watakapomenyana na Atletico Madrid. Barcelona wana mlima wa kukwea kutokana na kichapo cha mabao 2-0 nyumbani katika […]

MURANG’A SEAL YAMTIMUA KOCHA MONDAY

Klabu ya Murang’a Seal inayoshiriki ligi kuu ya soka nchini, KPL, imemfuta kazi kocha wake Osborne Monday, ikisema uamuzi huo uliafikiwa kufuatia makubaliano ya pande zote mbili. Kwenye taarifa rasmi, Seal pia ilithibitisha kumtimua naibu kocha mkuu Philip Wanjoya, na kumteua mchezaji wa zamani wa Harambee Stars Dennis Odhiambo kuwa kocha mkuu mshikilizi wanaposaka mkufunzi […]

K’OGALO, TUSKER KUCHUANA KATIKA DIMBA LA KPL

Matokeo ya mechi ya ligi kuu ya soka KPL kati ya Gor Mahia na Tusker FC hii leo yatasubiriwa kwa hamu na klabu ya AFC Leopards, Leopards na Gor Mahia wanapowania taji la ligi kuu hiyo. K’Ogalo wanaongoza ligi hiyo wakiwa na pointi 57 baada ya mechi 26, pointi 2 pekee mbele ya wapinzani wao […]

BABY PENDO: MAHAKAMA KUTOA MWELEKEO

Mahakama kuu ya Milimani jijini Nairobi imeratibiwa kutoa mwelekeo kuhusu uamuzi wa kuwaondolea mashtaka maafisa wakuu 8 wa polisi wanaohusishwa na ghasia za baada ya uchaguzi wa mwaka 2017 katika kaunti ya Kisumu ikiwemo mauaji ya mtoto Samantha Pendo maarufu kama Baby Pendo. Katika ombi lililowasilishwa mahakamani humo, familia ya Pendo, waathiriwa wengine wa ghasia […]