BINGWA SAWE AREJEA KWA MBWEMBWE
Shughuli za kawaida zilitatizika kwa muda katika uwanja wa ndege JKIA jana usiku wakati bingwa wa dunia katika mbio za marathon Sebastian Sawe kuwasili uwanjani humo kutoka London.
Sawe mwenye umri wa miaka 31 na mzaliwa wa Kijiji cha Ndonyongaria kaunti ya Nandi, alishangaza ulimwengu baada ya kuwa binadamu wa kwanza kukamilisha mbio hizo chini ya muda wa saa 2 Jumapili iliyopita.
Alipokelewa na maafisa wakuu serikalini akiwemo Waziri wa michezo Salim Mvurya.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 








































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































