MZOZO MWINGI: WASAFIRI WAKWAMA
Shughuli za uchukuzi zimeendelea kutatizika kwenye barabara kuu ya Mwingi kuelekea Garissa kutokana na hali tete ya usalama iliyochochewa na kuuawa kwa watu wanane mwishoni mwa wiki jana kwenye uvamizi.
Mzozo huo unaohusisha jamii mbili kutoka kaunti jirani, umesababisha kufungwa kwa barabara hiyo huku wasafiri wakikwama katika vituo vya mabasi ya usafiri.
Tayari muungano wa KUPPET umeitaka serikali kuhakikisha usalama wa walimu eneo la kaskazini mashariki.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 




























































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































