JAJI WARSAME NDIYE CHAGUO
Rais William Ruto anatarajiwa muda wowote kumteua rasmi jaji wa mahakama ya rufaa Mohammed Warsame kuwa jaji wa mahakama ya upeo, kufuatia kuteuliwa kwake hapo jana na tume ya huduma za mahakama, JSC.
Warsame ni miongoni mwa watu 5 waliohojiwa kwa muda wa siku mbili na JSC, mahojiano yake yakiendeshwa hapo jana kabla ya kuteuliwa kwake huku tume hiyo ikisema alionyesha uwezo mkubwa wa kuwa jaji wa mahakama ya upeo.
Jaji mkuu Martha Koome ni mwenyekiti wa JSC.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 




























































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































