RISING STARS WAKARIBISHWA KWA TAMASHA KUBWA
Timu ya taifa ya kandanda ya Kenya ya Vijana chini ya miaka 20, Harambee Rising Stars, imerejea nchini kwa makaribisho mema baada ya kufuzu kwa Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2025.
Timu hiyo ilijihakikishia nafasi yake kufuatia ushindi mkubwa dhidi ya Sudan na Burundi.
Kocha mkuu Salim Babu alionyesha kujivunia uchezaji wa timu hiyo lakini akabainisha haja ya maandalizi bora na ya mapema.
Kapteni Amos Wanjala alifurahia mafanikio yao.
Imetayarishwa na Nelson Andati
English 









































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































