SHUJAA WAPANGWA KUNDI GUMU BAADA YA HONG KONG

Timu ya taifa ya raga ya wachezaji 7 kila upande, Shujaa, imepangwa katika kundi jingine linaloonekana gumu katika mkondo ujao wa ubingwa wa SVNS duniani jijini Valladolid, utakaosakatwa tarehe 29-31 mwezi ujao. Shujaa watamenyana na Afrika Kusini, Australia, na Uingereza kwenye Pool A, na wataelekea kwenye mkondo huo baada ya kumaliza katika nafasi ya 7 […]

MWANAMME ADAIWA KUMWUA MWANAWE KWA UPANGA

Polisi katika kaunti ya Kakamega wanaendeleza uchunguzi katika tukio ambapo mwanamme mmoja katika Kijiji cha Emabusi eneo bunge la Ikolomani, ameripotiwa kumuua mwanawe kwa kumkatakata na kuwajeruhi wengine vibaya. Mwanamme huyo aliyeshambuliwa na wananchi wakati wa tukio hilo, anatibiwa hospitalini chini ya ulinzi mkali, huku walioshuhudia tukio hilo wkaisema alichukua hatua hiyo kutokana na mzozo […]

LINDA MWANANCHI YATOA MASHARTI KWA LINDA GROUND

Viongozi wa ODM wanaoegemea mrengo wa Linda Mwananchi unaoongozwa na katibu mkuu Edwin Sifuna wamesema kwamba wako tayari kushiriki mazungumzo na mrengo wa kinara Oburu Oginga, iwapo mrengo huo utakubali kuachilia nyadhifa za uongozi na kuruhusu uchaguzi mpya. Wakizungumza kwenye mkutano wa hadhara jijini Nakuru, Linda Mwananchi pia wamewataka wenzao wa Linda Ground kusitisha kampeni […]

MATIANG’I AKOSOA G2G

Mwaniaji wa urais kwa tiketi ya chama cha Jubilee Fred Matiang’i, ameikosoa serikali kutokana na kupanda kwa bei za mafuta, akihusisha ongezeko hilo na mpango wa uagizaji wa mafuta wa G2G anaosema haueleweki. Kwenye mahojiano na kituo kimoja cha runinga, Matiang’i ameitaka serikali kuweka wazi maelezo ya mpango huo, akitilia shaka hatua ya serikali kutolihusisha […]

RUTO ATETEA BEI ZA JUU ZA MAFUTA

Rais William Ruto ametetea bei ya juu ya mafuta nchini ikilinaginishwa na mataifa mengine katika Jumuiya ya Afrika Mashariki, akisema sababu ni kwamba Kenya inakuwa kiuchumi zaidi ya mataifa hayo. Akizungumza jijini Nairobi kabla ya kuelekea Italia kwa ziara ya siku 3, Ruto amesema kiwango cha miundomsingi ya barabara zilizojengwa nchini kinazidi kile cha mataifa […]

GACHAGUA: MAANDAMANO YA MAFUTA BADO JUMANNE

Muungano wa upinzani nchini umesisitiza kuwa maandamano ya kitaifa yalioratibiwa kufanyika hapo kesho kuishinikiza serikali kupunguza bei ya mafuta yangalipo. Ukiongozwa na kinara wa chama cha DCP Rigathi Gachagua, muungano huo umesema lengo la maandamano hayo ni kulalamikia gharama ya juu ya maisha itakayochangiwa na bei mpya za juu za mafuta. Aidha, amewahimiza vijana kusajiliwa […]

EPL: MAN U KUTOANA KIJASHO NA CHELSEA, ARSENAL KUKAZA NATI DHIDI YA MAN CITY

Ligi kuu ya uingereza inarejea wikendi hii kwa kishindo huku mbio za ubingwa zitazamiwa kuamuliwa. Hapo kesho Brentford watakua mbioni kusaka nafasi za ulaya wakiwakaribisha Fulham, Leeds wavaane na Wolves, Newcastle wakaribishe Bournemouth huku Tottenham wakipambana kujikwamua dhidi ya kushushwa daraja watakapomenyana na Brighton. Saa nne mechi kali ya siku itawahusisha Chelsea wakiwa Stamford Bridge […]

SHUJAA WAANGUKIA AUSTRALIA KWENYE MECHI YA UFUNGUZI

Timu ya taifa ya raga ya wachezaji saba Shujaa imeanza kampeni yake ya Hong Kong kwa kichapo cha alama kumi na nne kwa tano dhidi ya Australia katika mechi ya Kundi C iliyoonyesha mapungufu ya ulinzi pamoja na dalili za matumaini Australia walianza kwa kasi wakipata majaribio mawili ya haraka kupitia Josh Turner na James […]

MBIO ZA UBINGWA ZAZIDI KUPAMBA MOTO LIGI KUU

Mbio za ubingwa wa ligi kuu ya Kenya zinaingia hatua muhimu mwishoni mwa wiki hii huku mechi za ushindani mkali zikitarajiwa kuamua mwelekeo wa msimamo wa ligi AFC Leopards watachuana na mabingwa watetezi Kenya Police huku Gor Mahia wakipambana na Bandari walio katika kiwango kizuri hali inayoongeza presha kwa timu zinazowania ubingwa Ushindi wa hivi […]

KAKAMEGA HIGH WAJIPANGA KWA MASHINDANO YA RAGA YA WACHEZAJI SABA

Kocha mkuu wa raga wa shule ya Kakamega High Amos Wamanga amesema timu hiyo sasa imehamisha mwelekeo wake kuelekea mashindano ya wachezaji saba baada ya kumaliza katika nafasi ya nne kwenye mashindano ya kitaifa ya wachezaji kumi na watano Wamanga amesema timu ilijitahidi kadri ya uwezo wao katika mashindano hayo na kueleza kuridhishwa na kujituma […]