MECHI ZA EUROPA: ASTON VILLA WASAKA USHINDI

Michuano ya Ligi ya Europa itaandaliwa usiku wa Leo huku timu kadhaa zikipania kujiweka sawa katika mkondo wa kwanza wa mechi hizo. Saa tatu kasorobo itashuhudia mechi kadhaa ikiwemo Stutgart dhidi ya Porto, Bologna wavaane na Roma, huku Lille ya Ufaransa wakipambana na Aston Villa. Saa tano itashuhudia Nottingham Forest wakicheza dhidi ya Midjylland, Genk […]

NYABERI BADO ANA MATUMAINI YA KUPANDA DARAJA

Kocha wa Fortune Sacco FC, Vincent Nyaberi, amesema timu yake bado ina nafasi nzuri ya kupanda daraja kutoka Ligi ya National Super League licha ya kushika nafasi ya sita kwenye msimamo wa jedwali. Nyaberi amesema bado wana matumaini ya kumaliza miongoni mwa timu tatu bora ifikapo mwisho wa msimu. Matumaini hayo yaliimarika Jumamosi baada ya […]

BUYACHI: NIDHAMU ITASAIDIA OILERS KUISHINDA KABRAS

Kocha msaidizi wa Menengai Oilers, Lawi Buyachi, amesema utulivu na nidhamu vitakuwa muhimu timu yake itakapokutana na mabingwa Kabras Sugar RFC katika mechi ya Ligi ya Kenya Cup itakayochezwa Jumamosi katika uwanja wa Kakamega Showground. Timu ya Oilers kutoka Nakuru bado haijafanikiwa kuishinda Kabras katika mikutano 14 tangu ipandishwe daraja hadi ligi kuu katika msimu […]

MAHAKAMA YATUPILIA MBALI KESI INAYOPINGA UTEUZI WA NOORDIN HAJI

Mahakama Kuu imetupilia mbali ombi lililokuwa likipinga kuteuliwa kwa Noordin Haji kama Mkurugenzi wa Huduma ya Kitaifa ya Ujasusi (NIS) iKisema kuwa uamuzi wa Rais katika kuwateua maafisa wakuu wa umma ni wa hiari yake na unalindwa na Katiba. Katika uamuzi wake, mahakama iMEbainisha kuwa hoja za waliowasilisha kesi hiyo kwamba Haji hakupaswa kuteuliwa kutokana na […]

EACC YAWAHIMIZA WAKENYA KUKUMBATIA MFUMO WA FAINI ZA PAPO HAPO

Tume ya Maadili na Kupambana na Ufisadi (EACC) imewataka Wakenya kuunga mkono mfumo wa Mamlaka ya Kitaifa ya Usafiri na Usalama Barabarani (NTSA) wa kutoza faini za papo hapo kwa madereva wanaokiuka sheria za trafiki. Hata hivyo, wito huo unatolewa licha ya Mahakama kusitisha kwa muda utekelezaji wa mfumo huo kufuatia changamoto za kisheria zilizoibuliwa […]

WANAFUNZI 11 WAANGUKA NDANI YA SHIMO LA CHOO KAPSABET

Mwanafunzi mmoja amefariki na Wengine 10 wa Shule ya wasio na uwezo wa kusikia ya Kapsabet wamelazwa hospitalini baada ya kuanguka ndani ya shimo la choo lililoporomoka katika eneo la shule hiyo hilo wakati wanafunzi hao walipokuwa wakikimbilia kushuhudia msafara wa Rais William Ruto uliokuwa ukipita karibu na shule hiyo Wanafunzi hao walikuwa wamesimama juu ya shimo hilo lenye urefu wa takribani […]

WAKAZI WA KAPSABET WAOMBA UPANUZI WA BARABARA

Serikali imetakiwa kuchukua hatuza haraka na kupanua barabara kuu ya Kapsabet kaunti ya Nandi kuelekea Chavakali kaunti ya Vihiga, ili kuzuia visa vya ajali vinavyohusishwa na hali mbovu ya barabara hiyo. Wakizungumza mjini Kapsabet, wakazi, madereva na wahudumu wa boda boda wamelalamikia madai ya barabara hiyo kutelekezwa na idara husika, wakisema ni nyembamba mbali na […]

MAHAKAMA YASIMAMISHA FAINI ZA PAPO HAPO

Waendeshaji magari nchini wamepata afueni baada ya mahakama kuu kusimamisha utekelezaji wa mfumo wa mamlaka ya usalama barabarani, NTSA, kuwatoza faini za papo hapo wanapovunja sheria za trafiki. Kwenye uamuzi mapema leo, jaji Bahati Mwamuye ameizuia NTSA na afisi ya mwanasheria mkuu dhidi ya kutekeleza mfumo wa kuwatoza faini waendeshaji magari kwa njia yoyote ile […]

EACC, NG-CDF ZAJADILI KUZIBA UFISADI

Katika juhudi za kuziba mianya ya ufujaji wa fedha za umma katika hazina za kustawisha maeneo bunge, NG-CDF, tume ya maadili na kukabili ufisadi EACC inafanya kikao na maafisa wa NG-CDF kutoka magharibi mwa nchi. Mkutano huo unafanyika jijini Nakuru, mratibu wa EACC ukanda wa Magharibi Eric Ngumbi, akisema lengo ni kusaka suluhu kwa mianya […]

REAL WAITIA CITY KIKAONGONI, CHELSEA WAJIDHALILISHA UGENINI

Federico Valverde alifunga mara 3 na kuipa Real Madrid ushindi wa kushtua wa mabao 3-0 dhidi ya Manchester City, kwenye mkondo wa kwanza wa raundi ya 16 ya ligi ya klabu bingwa barani Ulaya. Vijana hao wa Alvaro Arbeloa walilipiza kisasi cha kichapo walichopokezwa Disemba mwaka jana katika uwanja huo wa Santiago Bernabeu, na kujiweka […]