FLICK KUSAINI MKATABA MPYA BARCELONA

Kocha wa klabu ya FC Barcelona Hansi Flick anatarajiwa kusaini mkataba mpya na klabu hiyo, baada ya mpango huo kuthibitishwa kufuatia kuchaguliwa tena kwa Rais Joan Laporta. Kwa mujibu wa taarifa hizo, mkataba mpya utadumu kwa miaka miwili ijayo, huku kukiwa na uwezekano wa kuongezwa hadi mwaka 2029 kupitia kipengele cha nyongeza. Inaarifiwa kuwa wakala […]

AMBANI: LEOPARDS BADO KATIKA MBIO ZA UBINGWA

Kocha mkuu wa AFC Leopards Fred Ambani amesema klabu hiyo bado iko kwenye mbio za ubingwa wa Ligi Kuu ya Kenya licha ya kuwa nyuma ya vinara Gor Mahia kwa pointi sita. Leopards kwa sasa wako nafasi ya pili wakiwa na Alama 55, kufuatia kipigo cha bao 1–0 katika mchezo wa Mashemeji Derby wiki iliyopita, Ambani akisema bado […]

BLADES WAJIANDAA KWA WIKENDI NGUMU BAADA YA MAANDALIZI KUHARIBIKA

Kocha mkuu wa timu ya Strathmore Blades Tony Ochieng amesema maandalizi ya timu yake kuelekea mechi za Ligi Kuu ya Mpira wa Kikapu kwa Wanaume nchini Kenya wikendi hii hayajakuwa mazuri kutokana na changamoto za hali ya hewa. Ochieng amesema timu imefanikiwa kufanya mazoezi moja pekee, huku wapinzani wao wakinufaika na kufanya mazoezi kwenye viwanja […]

RUTO AONGEZA KIMA CHA CHINI CHA MISHAHARA KWA WAFANYAKAZI

Rais William Ruto ametangaza ongezeko la asilimia 12 ya kima cha chini cha mishahara kwa wafanyakazi nchini pamoja na nyongeza ya asilimia 15 kwa wafanyakazi wa sekta ya kilimo. Ruto ametoa tangazo hilo wakati wa maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi yaliyofanyika katika kaunti ya Vihiga, akisema hatua hiyo inalenga kuboresha maisha ya wafanyakazi na kukabiliana […]

SERIKALI YATOA TAARIFA YA UCHUMI NA MAFURIKO

Msemaji wa Serikali Isaac Mwaura ametoa tathmini chanya kuhusu hali ya uchumi, huku akionya kuhusu hatari inayoongezeka ya mafuriko katika baadhi ya maeneo ya nchi. Katika taarifa kwa vyombo vya habari, Mwaura amesema kuwa Kenya ilizalisha ajira mpya 822,100 mwaka 2025, na kuongeza jumla ya walioajiriwa kutoka milioni 20.8 mwaka 2024 hadi milioni 21.6. Amebainisha […]

COTU YAISHINIKIZA SERIKALI KUHUSU MIKATABA YA KAZI

Katibu Mkuu wa COTU Francis Atwoli ameongeza shinikizo kwa Rais William Ruto kuharakisha kuridhia mikataba miwili muhimu ya kimataifa ya kazi, akionya kuwa kuchelewa kunadhoofisha ulinzi wa wafanyakazi pamoja na ahadi za serikali Akizungumza katika maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi kaunti ya Vihiga, Atwoli amesisitiza umuhimu wa serikali kuipa kipaumbele mikataba ya Shirika la Kazi Duniani, ikiwemo […]

MUTUA AELEZA MAFANIKIO YA AJIRA WAKATI WA MAADHIMISHO YA SIKU YA LEBA

Waziri wa Leba Alfred Mutua amesema kumekuwa na mafanikio makubwa katika sekta ya ajira nchini, akibainisha kuwa mamilioni ya nafasi za kazi zimezalishwa katika sekta mbalimbali. Akizungumza wakati wa maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi katika kaunti ya Vihiga, Mutua amesema utumishi wa umma umeunda ajira milioni 1.895 huku sekta ya biashara ndogo na za kati ikichangia ajira […]

MUDAVADI AUNGA MKONO RUTO 2027, ASISITIZA AWAMU MBILI

Mkuu wa Mawaziri  Musalia Mudavadi amesema kuwa tayari alionyesha mwelekeo wa kisiasa katika uchaguzi uliopita na kuwa msimamo huo bado haujabadilika kuelekea uchaguzi wa 2027. Mudavadi amesisitiza kuwa njia ni ile ile, akieleza wazi kuwa anamuunga mkono Rais William Ruto kuendelea kuongoza kwa muhula mwingine. Ameongeza kuwa ana imani kuwa Ruto atahudumu kwa mihula miwili, akiwataka […]

RUTO AKOSOA WANAOPINGA MIRADI

Rais William Ruto amewakosoa baadhi ya viongozi wanaopinga maendeleo ya miundombinu, akisema kauli zao hazina msingi na zinapotosha umma. Akizungumza wakati wa maadhimisho ya Leba kaunti ya Vihiga, Rais amesema kuna wanaodai kuwa barabara zinazojengwa hazina maana, licha ya manufaa yake kwa wananchi, na kushangaa kwa nini hawakutoa maoni wakati miradi ya barabara na reli ilipokuwa ikianzishwa. Aidha, […]

CHANGAMOTO ZA CBE ZAKATIZA NDOTO

Mfumo wa umilisi wa masomo, CBE unaendelea kukumbwa na changamoto huku maelfu ya wanafunzi wa Junior Secondary wakiripotiwa kuacha shule hali inayotia wasiwasi kuhusu utekelezaji wa mfumo mpya wa elimu nchini. Wadau wa elimu wanasema sababu kuu ni ukosefu wa miundombinu ya kutosha gharama za masomo pamoja na uhaba wa walimu wenye ujuzi maalum wa kufundisha […]

  • 1
  • 2