KOCHA WA LEVERKUSEN AHOJI MBINU ZA ARSENAL KWENYE MIPIRA YA KONA

Kocha wa Bayer Leverkusen Kasper Hjulmand amehoji uhalali wa mbinu za mipira ya set – piece zinazotumiwa na Arsenal kabla ya mechi ya kwanza ya hatua ya 16 bora ya Ligi ya Mabingwa Ulaya itakayochezwa hii leo nchini Ujerumani. Akizungumza katika mkutano na wanahabari Hjulmand ameuliza iwapo kuziba wapinzani wakati wa mipira ya kona kunafaa kuruhusiwa, hasa ikizingatiwa kuwa mbinu hizo zimekuwa […]

VIHIGA QUEENS WAJIANDAA KUKABILI MADIRA SOCCER ASSASSINS

Mabingwa mara nne wa Ligi Kuu ya Soka ya Wanawake ya FKF, Vihiga Queens, wamejipanga vyema kuelekea mechi yao dhidi ya Madira Soccer Assassins itakayochezwa Jumamosi katika Shule ya Upili ya Nyang’ori, kaunti ya Vihiga, ligi hiyo ikirejea baada ya mapumziko ya wiki mbili. Mapumziko hayo yalitokana na kambi ya timu ya taifa ya wanawake […]

KAIMOSI TTC WAWANIA UBINGWAWA MPIRA WA WAVU KANDA YA MAGHARIBI

Kocha wa timu ya mpira wa wavu ya Chuo cha Ualimu cha Kaimosi Geoffrey Lwangu amesema analenga kutwaa ubingwa wa kanda ya Magharibi huku mashindano hayo yakianza katika eneo la Lugari, kaunti ya Kakamega. Lwangu ameonyesha imani na uwezo wa kikosi chake kushinda wapinzani wao wakuu Bondo TTC, ambao waliwashinda kwa seti 3-2 katika fainali za mwaka uliopita. Akizungumza baada ya […]

MWENYEKITI WA KQ KIPRONO KITTONY AJIUZULU KUTOKA BODI YA NSE

Mwenyekiti mpya wa Bodi ya Shirika la Ndege la Kenya (KQ) Kiprono Kittony amejiuzulu kutoka bodi ya Soko la Hisa la Nairobi (NSE). Kittony anaondoka katika bodi ya NSE baada ya kuhudumu kwa takriban miaka sita tangu 2020. Kuondoka kwake kunafuatia kuteuliwa kwake Machi 1, 2026, kama mwenyekiti mpya wa shirika la ndege la Kenya […]

SEKTA YA UTALII KUUZA SERA ZAKE WAKATI WA MASHINDANO YA MAGARI

Bodi ya utalii nchini imesema kuwa itatumia vyema fursa ya mashindano ya mbio za magari ya Safari Rally Duniani (WRC) yaliyopangwa kuanza Alhamisi, ili kutangaza nchi hii kama kivutio kikuu cha utalii wa michezo. Bodi ya Utalii (KTB) imesema wageni zaidi ya 10,000 wanatarajiwa kuhudhuria mashindano hayo ya siku nne huko Naivasha, kilomita 90 kaskazini magharibi mwa mji […]

UEFA: BAYERN WATANGAZA UBAYA, LIVERPOOL WAKAANGWA

Kocha mkuu wa timu ya Liverpool Arne Slot, aliadhimisha mechi yake ya 100 kama mkufunzi wa klabu hiyo kwa kichapo, baada ya vijana wake kupoteza bao 1-0 dhidi ya Galatasaray jijini Istanbul, Uturuki katika mechi ya mkondo wa kwanza wa raundi ya 16 ya klabu bingwa bara Ulaya. Mbele ya kelele za mashabiki wa nyumbani, […]

KENYA YAZINDUA KIKOSI CHA MAKINDA WA GOFU

Zaidi ya wachezaji 100 wachanga wa mchezo wa gofu kutoka mataifa 15 barani Afrika watakongamana nchini kwa mashindano ya 2026 All-Africa Junior Team Championship, AAJTC, yatakayong’oa nanga tarehe 23 na kukamilika tarehe 26 mwezi huu jijini Nairobi. Mashindano hayo yatajumuisha vikosi kutoka mataifa kama vile Kenya, Ivory Coast, Nigeria, Botswana, Misri, Ghana, Mauritius, Namibia, Morcoo, […]

TIMU ZA NSL YAIMARISHA JUHUDI ZA KUINGIA KPL

Huku zikiwa zimesalia mechi 15 kabla ya kutamatika kwa kampeni ya National Super League nchini, timu za Mombasa United, Migori Youth FC na MOFA zimeonysha uwezo wa kupandishwa daraja kuingia ligi kuu ya KPL mwishoni mwa msimu. United inaongoza jedwali ikiwa na pointi 49, pointi 3 mbele ya Migori Youth huku MOFA wakishikilia nafasi ya […]

WAKENYA URUSI: OMTATAH KUISHTAKI SERIKALI

Seneta wa Busia Okiya Omtatah, ametangaza mpango wa kuwasilisha kesi mahakamani kuishtaki serikali kutokana na kinachoonekana kama kushindwa kuzuia mtandao wa ulaghai unaowasafirisha wakenya kupigana katika vita baina ya Ukraine na Urusi. Tangazo hilo linajiri huku familia kadhaa nchini zikiachwa na majonzi baada ya kushindwa kuwarejesha nchini jamaa zao waliofariki wakipigana kwenye vita hivyo. Omtatah […]

WIZARA YA AFYA KUTATUA CHANGAMOTO ZA SHA

Serikali imetoa hakikisho kwa walimu kwamba inashughulikia changamoto zote zinazowazuia kupata matibabu chini ya bima ya SHA, ambazo zilikuwa zimeibua hofu na shutuma miongoni mwa walimu. Waziri wa afya Aden Duale, amesema zaidi ya maafisa 400 wa afya wametumwa katika kaunti zote nchini kuangazia changamoto hizo kabla ya kuwasilisha ripoti. Haya yanajiri kufuatia vitisho vya […]