14 WAAGA, 16 WAJERUHIWA KWENYE AJALI WEBUYE

Watu 14 wameaga dunia huku wengine 16 wakiachwa na majeraha usiku wa kuamkia leo baada ya kugongwa na trela karibu na eneo la Malaha kwenye barabara kuu ya Webuye kuelekea Kitale. Kwa mujibu wa OCPD wa Webuye Rosemary Odeke, 14 hao waliaga dunia papo hapo baada ya kugongwa na trela hiyo, ripoti zikionyesha kuwa umati […]

HOWE AITAKA NEWCASTLE KUCHEZA MECHI YA MAISHA YAO

Kocha wa Newcastle United, Eddie Howe, ameitaka timu yake kutoa kiwango cha juu kabisa wakati watakaporushiana na FC Barcelona Jumanne katika mechi aliyoiita kuwa kubwa zaidi katika historia ya klabu. Newcastle watakuwa wakicheza hatua ya 16 bora ya UEFA Champions League kwa mara ya pili tu, wakikabiliana na vinara wa La Liga katika mkondo wa […]

KENYATTA UNIVERSITY WANYAKUA TAJI LA KUSF

Kenyatta University wamejinyakulia taji la soka la wanawake la Kenya Universities Sports Federation (KUSF) wakati wa mashindano ya International Women’s Day yaliyofanyika katika viwanja vya chuo kikuu cha Taita Taveta mjini Voi. Kenyatta University waliwashinda University of Eldoret mabao 2–0 katika fainali na kumaliza mashindano ya siku tatu bila kupoteza mchezo. Mabao ya Sheila Juma na Hope […]

KOCHA METTE ATOA TATHMINI KWA TUSKER FC

Kocha wa Tusker FC, Julien Mette, ametoa tathmini ya wazi kuhusu kikosi chake licha ya kuibuka na ushindi katika michezo miwili mfululizo iliyowasaidia kurudisha morali ya timu. Ushindi huo ni pamoja na 2–0 dhidi ya Bidco United katika FKF Mozzart Bet Cup, matokeo yaliyoihakikishia Tusker nafasi ya hatua ya 16 bora na kuendeleza msururu wa […]

ALIYEKUWA KOCHA HARAMBEE STARS ENGIN FIRAT AFARIKI DUNIA

Kocha wa zamani wa Harambee Stars, Engin Fırat, amefariki dunia kwa kifo cha ghafla kutokana na Mshtuko wa moyo akiwa na umri wa miaka 56. Fırat, aliyekuwa akiinoa makali klabu ya Nejmeh SC nchini Lebanon, aliripotiwa kuanguka katika uwanja wa ndege wa Istanbul, Turkey, alipowasili kutoka Beirut. Mashabiki wa soka nchini Kenya wanamkumbuka Fırat kwa kipindi chake na […]

SOKO LA UHURU LABOMOLEWA

Wafanyabiashara wadogo katika soko la wazi la Uhuru kando ya Barabara ya Jogoo wamepata hasara baada ya vibanda vyao kubomolewa usiku. Taarifa zinaonyesha kuwa tingatinga zilifika katika eneo hilo usiku wa jana  na kubomoa vibanda hivyo siku chache baada ya serikali ya Kaunti ya Nairobi kutoa notisi ya kuwaondoa wafanyabiashara hao. Hatua hiyo imejiri siku chache baada […]

MTU MMOJA AFARIKI AJALI YA BASI NAIROBI

Mtu mmoja amefariki huku wengine kadhaa wakijeruhiwa baada ya basi la abiria la City Shuttle kupoteza mwelekeo na kugonga magari kadhaa kwenye Barabara ya Valley, karibu na Hoteli ya Panafric jijini Nairobi. Ripoti za awali zinaonyesha kuwa basi hilo lilipoteza mwelekeo likishuka sehemu ya mteremko wa barabara hiyo na kugonga magari yaliyokuwa mbele pamoja na […]

WILLIS OTIENO AILAUMU SERIKALI KUHUSU MAFURIKO

Naibu kiongozi wa chama cha Safina na mwanasheria Willis Otieno amesema mafuriko yaliyokumba Nairobi na maeneo mengine nchini yamesababishwa na uongozi mbovu pamoja na ukosefu wa uwajibikaji katika mipango ya miji. Kupitia taarifa katika mtandao wa X, Otieno amesema mifereji mibovu na upangaji duni wa miundombinu umechangia vifo na uharibifu wa mali. Ameongeza kuwa wakazi […]

FAMILIA ZAIDI YA ELFU TATU ZAKABILIWA NA HATARI YA MAFURIKO

Familia zaidi ya elfu tatu katika kaunti nane za eneo la kati ziko katika hatari ya kukumbwa na mafuriko pamoja na maporomoko ya ardhi kufuatia mvua kubwa inayoendelea kunyesha. Kwa mujibu wa Shirika la Msalaba Mwekundu Kenya, tayari familia 48 zimeathirika msimu huu wa mvua huku shirika hilo likitoa wito kwa wakazi kuhama mapema kuelekea […]

OBURU ADAI ‘AJENDA 10’ ZIMETEKELEZWA

Kinara wa chama cha ODM Oburu Oginga amepuzilia mbali dhana kwamba ajenda 10 zilizoafikiwa baina ya chama hicho na UDA ikiwemo kuwapa fidia waathiriwa wa ukatili wa polisi hazijatekelezwa. Kwa mujibu Oginga, ripoti kuhusu ajenda hizo inaashiria matokeo ya mkataba huo katika sekta ya ugatuzi, anayosema imetengewa fedha zaidi, huku akidai kwamba tayari bunge limetenga […]