MFUMO MPYA WA FAINI ZA TRAFIKI WA NTSA WAPINGWA

Ombi limewasilishwa mahakamani kupinga mfumo mpya wa NTSA wa utoaji wa faini za papo kwa hapo kwa wanaokiuka sheria za trafiki, huku likitaka utekelezaji wake usimamishwe mara moja. Ombi hilo lililowasilishwa na Kennedy Maingi Mutwiri linajiri baada ya NTSA kutangaza kuwa mfumo huo mpya wa usimamizi wa faini za trafiki umeanza kutumika. Mlalamishi anadai mfumo huo […]

KRA KUWEKA KAMERA ZA MWILI KUZUIA HONGO FORODHANI

Maafisa wa KRA wataanza kuvaa kamera za miili kama sehemu ya mpango mpya wa kukabiliana na ufisadi unaolenga kudhibiti hongo na kula njama miongoni mwa wafanyikazi. Kamera za kuvaliwa mwilini zitatumiwa kimsingi na maafisa katika Idara ya Forodha na Udhibiti wa Mipaka. Imetayarishwa na Maurine Amwayi

SEHEMU YA BANDARI YA MOMBASA KUBINAFSISHWA, SERIKALI

Serikali kuu iko katika hatua ya mwisho ya kuwezesha sehemu za Bandari ya Mombasa na Lamu kusimamiwa na mashirika ya kibinafsi. Serikali imepanga kufuta sheria ya mamlaka ya bandari ya Kenya, KPA, ili kuondoa mamlaka hiyo na kuibadilisha kuwa Kampuni ya Umma yenye Hati ya Hisa (PLC) chini ya Sheria ya Kampuni, hatua ambayo itarahisisha uwekezaji wa sehemu ya […]

USIKU MKUBWA ULAYA, MECHI ZA AWAMU YA 16

Ni usiku mwingine wa kinyang’anyiro cha klabu bingwa bara Ulaya ambapo jumla ya mechi 4 za raundi ya 16 zitachezwa leo usiku, huku nyingine 4 zikisakatwa hapo kesho, ukiwa ni mkondo wa kwanza. Liverpool watarejea kikaangoni nchini Uturiki kumenyana na Galatasaray, walikocharazwa bao 1-0 katika awamu ya makundi msimu huu. Mechi nyingine itajumuisha Newcastle, ambao […]

RODRI APIGWA FAINI, APONEA MARUFUKU

Kiungo wa Manchester City na mshindi wa Ballon d’Or, Rodri, ametozwa faini ya pauni 80,000, sawa na takribani shilingi milioni 13.8 za Kenya kuhusiana na kauli zake alizitoa dhidi ya refa aliyesimamia mehi kati ya City na Tottenham mwezi jana. Kwenye kauli hizo, Mhispania huyo alikosoa hatua ya refa kuruhusu bao la Dominic Solanke, Rodri […]

CITY WAPEWA LIVERPOOL, ARSENAL WAPATA MTEREMKO FA

Manchester City wataialika Liverpool kwenye awamu ya robo fainali ya kipute cha FA Cup nchini Uingereza, kulingana na droo iliyofanyika jana usiku. Baada ya kuwashtua wengi na ushindi dhidi ya Sunderland, klabu ya Port Vale inayokabiliwa na hatari ya kushushwa daraja kutoka League One na ambayo ndiyo timu ya daraja la chini zaidi iliyosalia kwenye […]

FKF KUANDAA DROO YA FKF CUP

Shirikisho la soka nchini, FKF, linajiandaa kwa droo ya raundi ya 16 ya dimba la FKF Cup, baada ya raundi ya 32 kukamilika wikendi iliyopita. Tayari miamba kadhaa wa soka nchini ikiwemo AFC Leopards na Gor Mahia zimebanduliwa baada ya raundi 2 pekee, na timu ya BB Bread inayoshiriki ligi ya FKF tawi la Nairobi […]

AZIMIO YAWATIMUA WAASI

Muungano wa Azimio la Umoja One Kenya umeratibiwa kutangaza majina ya viongozi wapya wa muungano huo kujaza nafasi za viongozi waliofurushwa baada ya kujiunga na mirengo hasimu ya kisiasa au kuteuliwa serikalini. Miongoni mwa waliotimuliwa ni mbunge wa Suna East Junet Mohammed kutoka wadhifa wa kiongozi wa kundi la wabunge wa Azimio, nafasi yake ikijazwa […]

RUTO, WABUNGE WA ODM NA UDA KUPOKEZWA RIPOTI

Kamati inayosimamia utekelezaji wa mkataba uliotiwa saini na kinara mwanzilishi wa ODM marehemu Raila Odinga na Rais William Ruto kuhusu ushirikiano wa chama hicho na UDA, pamoja na ripoti ya mazungumzo ya kitaifa, NADCO, imeratibiwa kuwasilisha ripoti yake hii leo. Mwishoni mwa wiki jana, kamati hiyo maarufu kama Coin10, ilitangaza kukamilisha ripoti yake inapojiandaa kuiwasilisha […]

UPASUAJI WA MIILI YA MAFURIKO KUFANYWA 

Zoezi la upasuaji wa miili ya watu waliofariki kutokana na mafuriko wiki jana jijini Nairobi imeratibiwa hii leo katika makafani ya City, baada ya miili hiyo kutambuliwa huku idadi ya waliofariki kote nchini ikifikia watu 44. Familia za walioangamia zimekuwa zikifika katika makafani hayo tangu Jumamosi kwa lengo la kuwasaka na kuwatambua jamaa zao waliosombwa […]