WAKULIMA TRANS NZOIA WAPINGA RUZUKU YA MBEGU
Wakulima katika kaunti ya Trans Nzoia wametofautiana na mpango wa ruzuku kwa mbegu za mahindi uliotolewa na wizara ya kilimo wiki jana, wakisema bei zilizopunguzwa haziambatani na gharama ya uzalishaji wa mahindi.
Kwa mujibu wa wakulima hao, wizara ya kilimo ilipaswa kuwashirikisha kupitia vikao vya kukusanya maoni ili kubaini bei hitajika ya mbegu hizo.
Licha ya ruzuku hiyo kuonekana afueni, wakulima wameipinga.
Imetayarishwa na Antony Nyongesa
English 



















































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































