#Local News

COTU YAISHINIKIZA SERIKALI KUHUSU MIKATABA YA KAZI

Katibu Mkuu wa COTU Francis Atwoli ameongeza shinikizo kwa Rais William Ruto kuharakisha kuridhia mikataba miwili muhimu ya kimataifa ya kazi, akionya kuwa kuchelewa kunadhoofisha ulinzi wa wafanyakazi pamoja na ahadi za serikali

Akizungumza katika maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi kaunti ya Vihiga, Atwoli amesisitiza umuhimu wa serikali kuipa kipaumbele mikataba ya Shirika la Kazi Duniani, ikiwemo Mkataba wa 189 na 190

Ameeleza kuwa mikataba hiyo inalenga kulinda wafanyakazi wa majumbani pamoja na kukabiliana na vitendo vya ukatili na unyanyasaji mahali pa kazi, changamoto alizosema zimeenea na zinahitaji hatua za haraka kutoka kwa serikali.

Imetayarishwa na Cyrus Sifuna

Leave a comment

Your email address will not be published. Required fields are marked *