WAFANYIBIASHARA WEBUYE WALALAMIKIA AGIZO LA KENHA
Wafanyibiashara wanaoendesha shughuli zao katika soko la Dina mjini Webuye wamelalamikia hatua ya mamlaka ya ujenzi wa barabara kuu kuwataka waondoke katika sehemu wanayofanyia kazi.
Wakiongozwa na Abel Wanjala wamemtaka gavana wa Bungoma Ken Lusaka na mbunge wa sehemu hiyo Dan Wanyama kuingilia kati na kuwatengea sehemu maalum ya kufanyia biashara.
Imetayarishwa na Maureen Mukhobe
English 




























































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































