MARAGA ATAKA EACC KUICHUNGUZA SHA
Aliyekuwa jaji mkuu David Maraga anataka tume ya kupambana na ufisadi Eacc kupewa nafasi ya kuendesha uchunguzi katika fedha zilizodaiwa kupotea kupitia malipo kwa vituo bandia vya afya kupitia mamlaka ya SHA.
Maraga ambaye amezidi kukosoa jinsi mfumo wa SHA unavyotekelezwa anasema kumekuwa na juhudi za kuficha ukweli kuhusu mamilioni ya fedha zilizopotea.
Maraga amepuuzilia mbali hakikisho kutoka kwa waziri wa afya kuwa vituo vilivyojihusisha na ulaghai vilifungwa.
Imetayarishwa na Maureen Mukhobe.
English 




























































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































































